Misri yasaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi.

In Kimataifa

Wizara ya usafiri ya Misri imesaini makubaliano na kampuni za China katika kujenga reli nyepesi ya kasi yenye thamani ya dola bilioni 1.24 za kimarekani katika maeneo mapya mjini Cairo.

Reli hiyo mpya yenye urefu wa kilomita 66 na vituo 11, itaunganisha mji mkuu mpya wa utawala unaoendelea kujengwa na maeneo ya Cairo Kuu.

Waziri mkuu wa Misri Bw Sherif Ismail, waziri wa usafiri Bw Hesham Arafat pamoja na balozi wa China nchini Misri Bw Song Aiguo wamehudhuria hafla ya kusaini makubaliano kati ya Shirika la Usafiri la Misri NAT na kampuni ya usafiri wa anga ya China AVIC INTL na kampuni ya reli ya China.

Mkurugenzi wa shirika la usafirishaji la Misiri NAT amesema mradi wa reli hiyo utaanza ndani ya miezi miwili au mitatu, na inatarajiwa kusafirisha abiria laki 3.4 kwa siku.

Kampuni ya China, imesema ujenzi wa reli hiyo utatoa nafasi nyingi za ajira kwa Wamisri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu