Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ameagiza Mkandarasi anayekarabati kipande cha barabara ya Tanzania na Zambia

In Kitaifa

MKUU wa Mkoa wa Mbeya ameagiza Mkandarasi anayekarabati kipande cha barabara ya Tanzania na Zambia,TANZAM katika eneo la Simike jijini Mbeya kukamilisha kazi hiyo ndani ya juma moja , baada ya mradi huo kucheleweshwa kwa miezi sita, huku mkuu huyo wa mkoa akisema kuna umuhimu wa kuwepo kwa barabara mbadala za mzunguko jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Gabriel Makalla ametoa agizo hilo wakati wa ukaguzi wa kushtukiza ambao ameufanya baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi kutokana na msongamano wa magari kwenye eneo hilo.

Awali Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa wa Mbeya TANROADS amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa barabara hiyo imechelewa kutokana na changamoto mbalimbali ambayo ni pamoja na aiana ya lami inayotumika.

Mradi wa matengenezo ya kipande hicho cha barabara chenye urefu wa kilomita 1.7, unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.061,na ulisainiwa Mwezi Aprili mwaka jana na kuanza kazi mwezi Juni ,ambapo muda wa utekelezaji ni miezi tisa na ulitakiwa kumalizika machi 31 mwaka huu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu