Kocha wa Tottenham Jose Mourinho anahofu kuwa mshambuliaji wa kikosi hicho Harry Kane, 26 atakuwa nje ya uwanja mpaka msimu ujao na atakosa michuano ya Euro 2020 kutokana na jeraha.
Mourinho anahitaji washambuliaji wawili Januari hii kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Kane.
Mshambuliaji wa AC Milan Krzysztof Piatek, 24, ni mmoja kati ya wachezaji wanaotupiwa macho sambamba na mshambuliaji wa Napoli Fernando Llorente 34 na mshambuliaji wa Crystal Palace Christian Benteke, 29.