Mpango wa Brexit kufututiliwa mbali

In Kimataifa

Wabunge katika bunge la Umoja wa Ulaya wametoa wito kwa serikali ya Uingereza kufikiria vizazi vijavyo na kusalia katika Umoja huo. Katika barua ya wazi iliyonukuliwa na shirika la habari la Funke nchini Ujerumani, zaidi ya wabunge 100 wa Umoja huo wameitaka Uingereza iuache mchakato wa kuiondoa nchi yao maarufu kama Brexit. Wabunge hao wamesema uamuzi kama huo utapokelewa vyema katika Umoja wa Ulaya. Rasimu ya barua hiyo inatarajiwa kuchapishwa Uingereza leo kabla kura muhimu itakayopigwa katika bunge la Uingereza kuhusu rasimu ya mpango wa Brexit ya Waziri Mkuu Theresa May. Waangalizi wanasema May hana uungwaji mkono wa kutosha kwa rasimu hiyo kupita. Baadhi ya wabunge wa Uingereza wamependekeza kusogezwa mbele kwa siku ya mwisho ya Brexit ambayo ilikuwa imepangiwa kuwa Machi 29. Lakini mgombea mkuu wa chama cha European People’s Party, Manfred Weber amesema nyongeza hiyo ya muda haistahili kuvuka tarehe ya uchaguzi wa bunge la Ulaya mwezi Mei.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu