Mrithi wa Wenger kutangazwa kabla ya kombe la Dunia.

In Michezo

Klabu ya Arsenal inayoshiriki ligi kuu nchini Uingereza inatarajia kumtangaza kocha wake mpya atakae rithi mikoba ya Arsene Wenger kabla ya kuanza kwa michuano ya kombe la Dunia mwezi ujao nchini Urusi.

 

Wenger raia wa Ufaransa amesaliwa na michezo miwili kabla ya kumaliza kwa ligi na kuondoka ndani ya klabu ya The Gunners baada ya ufalme wake wa miaka 22 kufikia kikomo.

Timu hiyo mpaka sasa haijatangaza muda maalumu wa ujio wa kocha wao mpya lakini kwa mujibu wa tovuti yake imeandika kuwa kabla ya michuano ya kombe la Dunia kuanza Juni 14 ya mwezi ujao basi itakuwa ishamtambulisha.

Kocha wazamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique anahusishwa kujiunga na klabu hiyo akiwa sambamba na bosi wazamani wa Juventus, Massimiliano Allegri.

Wengine wanao husishwa na kupata dili la kuifundisha Arsenal ni pamoja na kiungo wake wazamani, Mikel Arteta na Patrick Vieira pia yumo kocha wa Monaco, Leonardo Jardim na mshindi mara tatu wa klabu bingwa barani Ulaya, Carlo Ancelotti.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu