Mshtakiwa wa mauaji ya mfanyakazi wake wa Ndani Mkami Shirima(30)Mkazi wa Sakina Arusha amefikishwa tena katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Arumeru akikabiliwa na shtaka la mauaji ya kukusudia.
Mtuhumiwa huyo aliyevuta hisia za wakazi wengi wa Jiji la Arusha waliokuwa mahakamani hapo kufuatilia kesi hiyo,alifikishwa mahakamani hapo akiwa chini ya ulinzi mkali wa Askari Magereza huku akiwa ameficha uso muda wote kwa kujifunika gubigubi na mtandio.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi April 8 mwaka huu kwa sababu ya upelelezi kutokamilika.