Mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa amewataka Watanzania kupuuza taarifa zilizorushwa na televisheni moja ya nchini Kenya kwamba Rais wa Tanzania, Samia Suluhu ameagiza wafungwa kwa kisiasa nchini kuachiwa huru.
Msigwa ametoa ufafanuzi huo leo Ijumaa Mei 7,2021 muda kabla ya kuanza kwa mkutano wa Rais Samia na wazee wa Dar es Salaam unaofanyika katika ukumbi wa Mlimani City.