Mkurugenzi wa uchaguzi katika manispaa ya ubungo Beatrice
Domonic, amegoma kutoa fomu kwa mgombea ubunge wa
Chadema, akieleza kuwa tayari chama hicho kilishachukua fomu
hiyo kupitia kwa mgombea mwingine aliyetambulika kwa jina la
Athumani Abdala Sudi wa kibamba.
Songombingo hilo limejitokeza mara baada ya chadema kufika
katika ofisi za Mkurugenzi huyo, wakitaka kuchukua fomu na
Mgombea wao, na ndipo walipopewa taarifa kuwa tayari yupo
Mgombea wa chama hicho ambaye ameshachukua fomu na kwa
utaratibu wa tume fomu hazitolewi mara mbili kwa chama kimoja.