Msumbiji yasema hali inaanza kuwa nzuri kuwezesha zoezi la kusambaza msaada

In Kimataifa

Serikali ya Msumbiji imesema hali katika maeneo yaliyokumbwa na kimbunga Idai imeanza kuwa nzuri kuruhusu msaada wa dharura kupelekwa haraka kwa watu wanaouhitaji. Imesema barabara muhimu inayoelekea katika mji wa Beira hivi sasa imefunguliwa, na msaada wa kimataiafa unaanza kumiminika. Jeshi la Marekani limesema litaungana na mashirika ya kimataifa ya wahisani katika kusambaza madawa na chakula kwa waathiriwa wa kimbunga hicho kilichosababisha maafa makubwa ya kiasili kuwahi kuukumba ukanda wa Kusini mwa Afrika kwa miongo mingi. Waziri wa mazingira wa Msumbiji Celso Correia amesema watu 228,000 wamewekwa katika kambi katika eneo kubwa la Msumbiji lililofurika. Kumeripotiwa mripuko wa magonjwa ya kuhara, lakini waziri Correia amesema bado ni mapema kujua ikiwa ugonjwa huo ni kipindupindu. Idadi ya waliopoteza maisha kutokana na kimbunga Idai imefika watu 761, kati ya hao 446 wakiwa kutoka Msumbiji, 259 kutoka Zimbabwe, na 56 wakiwa Wamalawi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu