Mtumishi serikalini akamatwa na jeshi la polisi kwa kile kinachodaiwa ni kuchochea maandamano

In Kitaifa

Jeshi la polisi mkoani Dodoma limemkamata na mfanyakazi mmoja wa mfuko wa afya wa NHIF kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano kwenye mitandao ya kijamii yanayoratibiwa na mwanamke maarufu mitandaoni ajulikanaye kwa jina la Mange Kimambi.

Tokeo la picha la Gilles Muroto

Kamanda Gilles Muroto

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Machi 21, 2018, Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Kamishna msaidizi Mwandamizi, Gilles Muroto amesema jeshi hilo limemshikilia mtumishi huyo wa NIHF na mwenzake mkazi wa Bahi kwa makosa ya kuchochea maandamano.

Akitaja majina ya waliyoshikiliwa Kamanda Muroto amesema kuwa ni AMANI CHARI, ambaye ni mfanyakazi wa mfuko wa Taifa wa bima ya afya – NHIF na Yuda Mbata ambaye ni mkazi wa wilayani Bahi.

Kwa upande mwingine, Kamanda Mruto amewaonya watu kutofuata mkumbo wa kuhamasisha maandamano iwe kwa njia ya mitandao au njia yoyote ile kwani kufanya hivyo ni kosa kisheria .

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu