Mufti mkuu wa Tanzania, Aboubakary Bin Zubeir, leo Machi
18, amezungumza na waandishi wa habari kuhusiana na
mlipuko wa ugonjwa wa Corona, ambao mpaka sasa wagonjwa
wamefikia watatu.
Ameyasema hayo kutoka jijini Dar Es Salaam mapema leo kwa
lengo la kuzuia mikutano inayokusanya waumini wa dini ya
Kislam hapa nchini kwa lengo la kuzuia maambukizi ya virusi
vya Corona.