Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakari Zubery Bin Ally
amewaomba watanzania kuungana kwa pamoja kumuomba
mwenyezi Mungu ili virusi vya ugonjwa wa Corona visiendelee
zaidi na kuzua hofu ya kushindwa kufanya Ibada katika mji
mtakatifu wa Maka na Madina nchini Saudi Arabia.
Antenna imenasa Mufti Abubakary Zubery akisema hayo
mapema leo ofisini kwake jijini Dar Es Salaam.