Museveni atilia shaka uraia wa mawaziri wake.

In Kimataifa

Rais Yoweri Museven wa Uganda amesema kuwa baadhi ya mawaziri wake si raia wa Uganda.

Museveni amemtaja waziri wa nchi anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Julius Wandera Maganda kuwa mmoja wa mawaziri ambao si raia wa Uganda.

Maganda na Aggrey Awori ambaye kutoka mwaka 2009 hadi 2011 alikuwa waziri wa Habari na Mawasiliano, wanatoka Busia, wilaya ya mpakani na Kenya na ni kilomita 196 mashariki mwa Kampala.

Museveni aliongeza kwamba wala hajui wanakotoka mawaziri wengine, kwa sababu kila anapowauliza huwa hawamwambii.

Alisema yote hayo kuonyesha mwingiliano wa kihistoria, utamaduni na lugha miongoni mwa watu wa nchi sita wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu