Mvua zinazoendelea kunyesha zaleta Balaa

In Kimataifa

Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbali mbali Duniani zimeleta Madhara makubwa katika mji wa Edgecumbe uliopo kaskazini mwa nchi ya New Zealand.

Maelfu ya wakazi wameyakimbia makazi yao baada ya mafuriko makubwa yaliyozunguka mji huo kutokana na mvua kubwa iliyosababishwa na kimbunga cha Debbie kuyafunika makazi yao.

Kimbuka hicho pia kiliiathiri nchi ya Australia Alhamisi ya wiki iliyopita na kusababisha mito mbalimbali katika nchi hiyo kujaa kingo zake.

Katika mji wa Edgecumbe maji yanasemekana kufika hadi mita 2 katika baadhi ya maeneo. Hata hivyo hakuna ripoti yoyote ya kifo katika mafuriko hayo lakini kuna mtu mmoja ambaye alikuwa katika mto ndio anatafutwa na mpaka sasa hajaonekana.

Polisi katika mji huo wamesema watapiga doria katika maeneo yaliyohamwa na kuweka vizuizi kuwazuia raia wasije wakarudi. Tazama picha za mafuriko katika mji huo hapa chini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu