Waziri wa utamaduni sanaa na michezo Harson Mwakembe leo amempokea miss Word katika shule ya sekondary Moshono iliyopo kata ya Moshono Jijini Arusha
Akizungumza na vyombo vya habari waziri Mwakembe amesema kuwa, ujio wa mrembo huyo ni mojawapo ya fursa ya kutangaza sekta ya utalii hapa nchini na kujitangaza duniani kwenye mataifa mbalimbali
Mkurugenzi wa uendeshaji wa mashindano ya miss Tanzania Basila Mwanukuzi ambaye alikuwa miss Tanzania mwaka 1998 amesema kuwa wameandaa technolog ya kuandaa taulo za kike kwa kushirikiana na miss Dunia na Miss Tanzania katika baadhi ya shule hapa nchini kwani hii inasaidia kuwafanya waweze kuendelea na masomo yao bila kubugudhiwa
Nao baadhi ya wadau walioshiriki katika zoezi la ugawaji wa taulo za kike akiwemo mwenyekiti wa kampuni ya Uhuru Pad Sarah Gunda wamesema wameshukuru kwa ushirikiano walioupata ambapo wameahidi kuendelea na project ya kutoa elimu kwa watoto wa kike na ugawaji wa taulo za kike
Kwa upande wake Miss word Vanesa Ponce ameshukuru kwa kuja Tanzania ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na vijana wa kike katika kusambaza taulo za kike mashuleni
Hata hivyo Mrembo huyo ameendesha zoezi la kugawa taulo za kike sambamba na upandaji wa miti katika shule ya sekondary Moshono