Mwalimu mkuu amcharaza viboko mwalimu mwenzake.

In Kitaifa

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Migango wilayani Biharamulo, amemchapa viboko mwalimu mwenzake mbele ya wanafunzi akimtuhumu kwa wizi wa sahani tano, pamoja na nusu kilo ya sukari iliyotolewa kwa ajili ya mahafali ya wahitimu wa darasa la saba.
Katika taarifa yake ya kulaani kitendo hicho, kaimu katibu wa Chama cha Walimu Tanzania CWT Wilaya ya Biharamulo Joseph Lugumba amesema kuwa, mwalimu mkuu Mateso Musaku alimpiga viboko mwalimu wake Hosea Masatu mbele ya wanafunzi, tukio ambalo linalaaniwa vikali.
Lugumba amesema baada ya kupata taarifa za mwalimu huyo kuchapwa viboko uongozi wa CWT ulifika shuleni hapo kujiridhisha, ambako wanafunzi na wazazi walithibitisha tukio hilo, ikidaiwa kwamba mwalimu huyo alifungwa kamba kwenye mti.
Amesema mwalimu Masatu alidaiwa kuiba vitu hivyo siku moja baada ya kumalizika mahafali ya darasa la saba, na kwamba alipoulizwa alikiri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu