Mwanahabari wa Urusi aliyeikosoa serikali auawa mjini Kiev.

In Kimataifa

Mwandishi habari wa Urusi aliyekuwa mkosoaji mkubwa wa kile alichokiita kuwa ni vitendo vya uchokozi vinavyofanywa na Urusi nchini Georgia, Crimea, Mashariki mwa Ukraine na Syria, alipigwa risasi jana mgongoni nyumbani kwake mjini Kiev. Arkady Babchenko alifariki dunia wakati akipelekwa hospitali. Polisi ya Ukraine imesema mke wake alimkuta akiwa chumbani akivuja damu. Babchenko aliyekuwa na umri wa miaka 41, aliondoka Urusi mwaka wa 2017, akikabiliwa na miito ya kupokonywa uraia wake na kuongezeka kwa vitisho dhidi yake kutokana na maoni yake kuhusu ajali ya ndege ya Desemba 2016 ambayo iliwauwa waimbaji wa kwaya ya heshi la Urusi waliokuwa njiani kwenda Syria kuwatumbuiza marubani wa jeshi. Alituhumiwa kwa kukosa uzalendo, kitu alichosema kuwa kinashangaza ikizingatiwa kuwa aliipigania nchi yake katika vita vya kwanza ya kutaka kujitenga nchini Chechnya katika miaka ya 1990. Wanasiasa wanaoiunga mkono serikali walianza kumkana na kutaka afungwe jela kutokana na maoni yake.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu