Mwili wa Msanii Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ umewasili nyumbani kwao katika Kijiji cha Utengule mkoani Mbeya tayari kwa mazishi.
Mara baada ya kuwasili kwa mwili huo, vijana wa Green Guard wa Chama cha Mapinduzi ndiyo walioubeba mwili huo kutoka ndani ya gari hadi ndani ya nyumba yao marehemu.
Wasanii mbalimbali wamemsindikiza mwenzao wakitokea jijini Dar Es Salaam.
Msanii huyo aliyefariki Ijumaa iliyopita na kuagwa jana kwenye viwanja vya LEADERS Mazishi yanatarajiwa kufanyika mchana huu.