Mwili wa Savimbi wagombaniwa.

In Kimataifa

Mzozo umeibuka baina ya serikali ya Angola na upinzani juu ya mipango ya kuzika upya mwili wa aliyekuwa kiongozi wa vugugu la waasi wa Unita ambaye kifo chake kilitokea miaka 17 iliyopita na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa karibu miongo mitatu.

Serikali ilikuwa inataka kuukabidhi mwili wa Savimbi kwa wawakilishi wa Unita, ambacho sasa ni chama cha upinzani, ili waweze kuuzika mwili wake nyumbani kwao tarehe Mosi Juni.

Hata hivyo, makabidhiano ya mwili hayakufanyika na kila upande sasa unamlaumu mwingine.

Helena Savimbi, mmoja wa watoto wa kike wa kiongozi huyo wa waasi ameliambia shirika la habari la AFP kwamba serikali haikuheshimu mkataba. “Ni mkanganyiko mkubwaIt’s ,” alinukuliwa akisema.

Serikali nayo imeishutumu Unita kwa kushindwa kuuchukua mwili Jumanne, kama walivyokubaliana.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu