Kikosi cha Namungo FC kinachonolewa na Kocha Mkuu,
Hemed Moroco leo Aprili 12 kimerejea Tanzania kikitokea
nchini Zambia ili kuendelea na mechi zake za Ligi Kuu Bara.
Namungo jana Aprili ilikuwa na kibarua cha kuipeperusha
Tanzania kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya
Nkana FC.
Mchezo huo dakika 90 zilikamilika kwa Nkana FC kushinda bao
1-0 dhidi ya Namungo na kufanya kikosi hicho kilicho kwenye
kundi D kupoteza mechi zake mbili mbele ya Nkana FC.
Ule wa kwanza walipokutana Uwanja wa Mkapa, ubao ulisoma
Namungo 0-2 Nkana FC. Kwenye kundi D Namungo FC ipo
nafasi ya nne bado haijakusanya pointi.