Ndege yatua kwa dharura kwenye shamba la mahindi…

In Kimataifa

Ndege ya abiria ya Urusi imelazimika kutua kwa dharura kwenye shamba la mahindi karibu na jiji la Moscow baada ya kugonga kundi la ndege.

Watu ishirikini na watatu wamejeruhiwa katika tukio hilo, ambalo limesababisha ndege kutua huku injini yake ikiwa imezima na gia yake ya kutua ikipata hitilafu.

Ndege hiyo Ural Airlines Airbus 321 ilikuwa ikisafiri kuelekea katika eneo la Simferopol Crimea ilipogonga kundi la ndege muda mfupi baada ya kuondoka uwanjani, hali iliyovuruga utendaji wa injini yake.

Vyombo vya habari vya taifa la Urusi vimetaja kutua kwa ndege hiyo kama muujiza wa eneo la Ramensk.

Maafisa wa ndege hiyo wamesema ndege imeharibika sana na haiwezi kupaa tena,na uchunguzi rasmi juu ya ajali hiyo unaendelea.

Ndege hiyo ilikwa na abiria 233 na wahudumu ndani yake, wakati ndege waliporipotiwa kuingia ndani ya injini na rubani wake akaamua kutua mara moja kwenye shamba la mahindi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu