Ndugai Amtimua Bungeni Mbunge

In Kitaifa

Spika wa Bunge , Job Ndugai amemtimua bungeni mbunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuvaa suruali inayombana.

Mbunge huyo wa Momba Condester Sichwale alitimuliwa bungeni na Spika, kulingana na kanuni za Bunge, ambazo zinawataka wabunge wanawake kutovaa suruali za kubana.

Hatua ya kufukuzwa bungeni kwa Mbunge Sichwale imekuja baada ya mbunge wa CCM wa Nyang’wale Hussein Amar kusimama na kuomba mwongozo wa Spika, huku akisema kuwa kuna wanawake waliokiuka kuvaa mavazi ya staha.

Spika Ndugai alimpa nafasi mbunge huyo kumtaja mwenzake aliyevaa mavazi ambayo hayakuwa na staha ili iwe mfano na ndipo alipoashiria alipokaa mbunge huyo bila kumtaja jina.

Hatahivyo Spika alisimama na kumtaka mbunge aliyevaa mavazi hayo asimame na aondoke ndani ya ukumbi ili akavae mavazi yenye staha ndipo atarejea tena bungeni.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu