NEC YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO.

In Kitaifa

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa madiwani kwenye kata sita (6) zilizopo kwenye halmashauri sita (6) katika mikoa sita (6) ya Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa Tume Jaji (Rufaa) Semistocles Kaijage amesema Jijini Dar es Salaam leo (Jumanne 09.04.2019) kwamba uchaguzi huo utafanyika tarehe 19 Mei mwaka huu.
Akisoma taarifa kwa umma iliyotolewa na Tume, Jaji Kaijage amesema kwamba fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kati ya tarehe 15 hadi tarehe 19, Aprili mwaka huu.
Aidha Mwenyekiti huyo wa Tume amesema kwamba uteuzi wa wagombea pia utafanyika tarehe 19, Aprili mwaka huu na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 20, Aprili hadi tarehe 18 Mei mwaka huu.
Alifafanua kwamba uchaguzi katika kata hizo, utafanyika sambamba na Uchaguzi Mdogo wa

Ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki . “Tume inapenda kuvikumbusha Vyama vya Siasa na wadau wote wa Uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi, Taratibu, Miongozo na Maelekezo yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati wa kipindi chote cha Uchaguzi huu mdogo,” alisema Jaji Kaijage.

Awali Jaji Kaijage alisema kwamba maamuzi ya kutangaza uchaguzi kwenye kata hizo yamefanyika baada ya Tume kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa ambaye kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 aliitaarifu Tume juu ya uwepo wazi wa nafasi hizo.

Alisema kwamba nafasi hizo wazi zimetokana na vifo vya Madiwani watano (5) na mmoja (1) kujiuzulu.

Kata hizo ni pamoja na Uwanja wa Ndege iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi, Kitobo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera, Kyela iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya, Mikocheni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mkoani Dar es Salaam, Mvuleni iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Mkoani Lindi na Manda iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu