Mshambuliaji nyota wa timu ya taifa ya Brazili na klabu ya PSG, Neymar Jr hapo jana amewasili nchini kwao kwaajili ya upasuaji wa kifundo chake cha mguu.
Hali ya Neymar bado tata, Kurudishwa kwao Brazili
Neymar ambaye alipata majeraha katika mchezo wa juma lililopita dhidi ya Marseille ametua katika uwanja wa ndege wa Brazili hapo jana siku ya Alhamisi huku akitumia baiskeli ya magurudumu mawili ‘wheelchair ‘ yanayomsaidia kusonga mbele.
Nyota huyo ghali zaidi kwa sasa duniani anatarajiwa kusafirishwa hadi Belo Horizonte mahala ambapo atapatiwa upasuaji.
Daktari wa timu ya taifa ya Brazili, Rodrigo Lasmar amesema kuwa hewanda Neymar akawa nje ya uwanja kwa takribani miezi mitatu.
Daktari wa timu ya taifa ya Brazili, Rodrigo Lasmar akizungumzia hali ya Neymar
Neymar amevunjika mfupa muhimu sana katika kifundo cha mguu na operesheni yake itafanyika katika Belo Horizonte siku ya Jumamosi asubuhi na kupona kwake kutachukua miezi miwili na nusu hadi mitatu.
Nafahamu Neymar anajiskia vibaya ila hamna jinsi kwa sasa na itataria nay eye mwenyewe ilikuweza kupona haraka. Tutafanya kazi yetu kwa kiwango cha hali ya juu aliaweze kupona haraka.