Ndoa ya msanii maarufu wa muziki nchini Marekani, Nicki Minaj na mchumba wake Kenneth Petty imeanza kufukuta kwani tayari Nicki Minaj ameonesha kila dalili kuwa wawili hao kwa sasa wanasubiri muda tu wafunge ndoa.
Tayari Nicki Minaj ameonesha dalili hizo kwa kuanza kubadilisha jina lake kwenye ukurasa wake wa Twitter na kujiita Mrs. Petty, Kitendo cha kubadili jina lake, Kimeleta maswali mengi kwa mashabiki wake wengi wakiamini kuwa tayari wawili hao wamefunga ndoa kimya kimya.
Wiki iliyopita wawili hao walipata kibali cha kufunga ndoa ndani ya miezi mitatu, Taarifa ambazo Nicki Minaj mwenyewe alizithibitisha kwenye mahojiano yake na Podcast ya Joe Budden.