Njiwa aliyetumiwa kusafirisha mihadarati apigwa risasi.

In Kimataifa

Polisi nchini Argentina wamempiga risasi njiwa ambaye alitumiwa kusafirisha mihadarati kwenda gereza moja nchini humo, kwa mujibu wa mamlaka za gereza hilo.

Njiwa huyo alionekana akiruka hadi kwenye uwanja wa gereza hilo, lililo katika mji wa Santa Rosa.

Maafisa waligundua kuwa ndege huyo alikuwa amefungiwa mfuko mdogo kwenye mgongo wake, uliokuwa na vidonge vya madawa ya kulevya.

Njia hiyo ya kusafirisha madawa ilikuwa imegunduliwa, na ilikuwa ikifanyiwa uchunguzi.

Gazeti la Clarin lilichapisha picha ya njiwa huyo akiwa na mfuko mweupe, uliokuwa na tembe 44 za madawa ya kulevya.

Magereza nchini Argentina yalionya mwaka 2013 kuwa, walanguzi wa madawa ya kulevya walikuwa wakitumia njiwa waliokuwa wakifanya safari mara 10 hadi 15 kwa siku.

Watu watatu walikamatwa na njiwa 15 kupatikana, baada ya uchunguzi wa mwaka 2013.

Mapema mwaka huu njiwa ambaye alikuwa na mfuko uliokuwa na tembe 178 za dawa ya kulevya, alishikwa nchini Kuwait karibu na mpaka na Iraq.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu