Nondo apewa dhamana Iringa.

In Kitaifa

Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Iringa kupitia kwa Hakimu wake John Mpitanjia imeweka wazi dhamana kwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo.

Hakimu Mpitanjia ametoa masharti ya dhamana hiyo kwa Nondo ni kuwa na watu watakao mdhamini ambao ni wakazi wa Iringa, mmoja awe anafanya kazi serikalini, wawekebondi ya shilingi milioni tano na wawe na mali isiyohamishika.

Hata hivyo wakili wa Nondo, Jebra Kambole anashughulikia dhamana hiyo. Wakati huo huo kesi hiyo imeahirishwa mpaka April 4 ya mwaka huu.

Nondo anashtakiwa kwa makosa mawili ikiwemo kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni March 7 ya mwaka huu kuwa maisha yake yapo hatarini akiwa katika eneo la Ubungo na kuzisambaza kwenye mtandao wa Whatsapp.

Kosa la pili limetajwa kuwa ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma Mafinga wakati alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha polisi mjini humo kwa kusema kuwa alitekwa na watu wasiojulikana.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu