Nyalandu asema sababu za kuelekea Chadema.

In Kitaifa, Siasa

Aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini CCM Lazaro Nyalandu, amesema ni kwa nini ameamua kutaka kujiunga chadema na sio chama kingine cha siasa hapa nchini.
Nyalandu ambaye amewahi kuwa naibu waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara na baadaye Maliasili na Utalii kabla ya kuwa waziri kamili, alitangaza uamuzi wa kuhama CCM Jumatatu.
Moja ya sababu alizozieleza ni kutoridhishwi na mwenendo wa kisiasa nchini, ukiukwaji wa haki za binadamu, dhuluma na mihimili miwili ya nchi kushindwa kufanya kazi yake kwa uhuru.
Amesema kuhama CCM ni kitu kilichomchukua muda mrefu, kutokana na yanayoendelea ndani ya chama hicho tawala,na hapa anaeleza kwa nini ameamua kuelekea CHADEMA.

Pia Nyalandu amesema uamuzi wake wa kujitoa CCM ni moja ya mambo matatu makubwa aliyofanya maishani hadi sasa.
Uamuzi wa kwanza ukiwa ni wa kumfuata Yesu Kristo awe mwokozi wa maisha yake, wa pili kuamua mwanamke gani awe mke wake na watatu ni huo wa kuamua kuachana na CCM.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu