Kiungo wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria na club ya
Chelsea ya England John Obi Mikel amefikia hatua ya kuvunja
mkataba wake na club yake ya Trabzonspor ya nchini Uturuki.
Uamuzi huo umekuja ikiwa ni siku chache zimepita toka kiungo
huyo atupe lawama wa shirikisho la soka nchini Uturuki kwa
kushindwa kusimamisha Ligi wakati huu wa mlipuko wa virusi
vya corona.
Obi anadaiwa kuwa Jumapili ya March 16 2020 zikiwa Ligi
mbalimbali duniani zimesimama kwa hofu ya corona, anadaiwa
kuwa aligoma kucheza katika mchezo dhidi ya Basaksehir.
Sababu rasmi za kuvunjwa kwa mkataba huo hazijawekwa ila
Obi hatopokea fidia yoyote kwani yeye ndio aliyeomba, hadi
sasa zaidi ya wachezaji watano Wakubwa Ulaya wamethibitika
kupata maambukizi.