Papa Francis awasili kwa ziara ya historia katika Umoja wa Falme za Kiarabu UAE.

In Kimataifa

Papa Francis amewasili katika Umoja wa falme za kiarabu kwa ziara ya kwanza kuwahi kufanyika na kiongozi mkuu katika kanisa katoliki Roma, katika rasi ya Arabuni.

Alitua mjini Abu Dhabi ambako alikaribishwa na mwanamfalme Sheikh Mohammed bin Zayed al-Nahyan.

Papa anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa dini mbali mbali na Jumanne aandae misa ambapo takriban watu 120,000 wanatarajiwa kuhudhuria.

Kabla ya kuondoka alielezea wasiwasi wake kuhusu vita nchini Yemen ambapo Umoja wa Falme za kiarabu umehusika.

“Raia nchini Yemen wamechoshwa na mzozo wa muda mrefu na watoto wengi wanateseka kwa njaa, lakini hawawezi kufikia maghala ya chakula ,” Papa amesema

“Kilio cha watoto na wazazi wao kinapaa mbinguni kwa Mngu,” aliongeza.

Haijulikani wazi iwapo anapanga kulizusha suala hilo mbele ya umma au katika faragha wakati wa ziara yake. Umoja wa Falme za kiarabu unahusika katika mzozo nchini Yemen kama sehemu ya muungano unaoongozwa na Saudia.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu