Staa wa soka wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amewasili mjini Turin Italia kwa ajili ya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na club ya Juventus ya Italia, hiyo ikiwa ni siku chache zimepita toka Juventus wafikie makubaliano na Real Madrid.
Ronaldo amewasili Turin kwa ajili ya kukamilisha usajili wake ambapo atasaini Juventusmkataba wa miaka minne na Jumatatu ya July 16 2018 atatambulishwa rasmi kama mchezaji wa Juventus kwa dau la usajili la euro milioni 100 huku Real Madridwakikubaliana na Juventus kuongezewa euro milioni 12 katika kipindi cha miaka miwili.