Polepole asema ccm sasa ni chama cha wananchi wote.

In Kitaifa

KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amesema zama za watu wachache wenye fedha chafu, kuhonga wanachama na kuweka viongozi wanaowataka, zimekwisha.

Amesema CCM sasa ni chama cha wanachama wote kama Katiba inavyosema, bila ya kujali rika wala rangi na wenye kutaka uongozi ndani ya chama kwa kutumia fedha chafu, chama hakitasita kuwachukulia hatua ikiwamo kukata majina yao.

Kiongozi huyo wa CCM ameyasema hayo mkoani Arusha alipokutana na viongozi wa chama wa Wilaya ya Arusha ,kutoka kata zote 25 wakiwemo wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Arusha.

Aidha amewataka wanaCCM kuwataja viongozi wanaotaka uongozi ,kwa kugawa fedha chafu ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao.

Polepole amewataka wakazi wa Arusha kutorudia makosa yaliyojitokeza katika uchaguzi zilizopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu