R. Kelly akabiliwa na mashtaka mapya 11 ya unyanyasaji wa kingono.

In Burudani

R.Kelly ameshtakiwa kwa makosa 11 ya unyanyasaji wa kingono, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini Marekani.

Mahakama imeripotiwa kuonyesha kuwa vitendo hivyo vilifanywa dhidi ya watoto wa umri kati ya miaka 13 na 16, na ikiwa itathibitika atakabiliwa na adhabu kali kuliko adhabu nyingine anazokabiliwa nazo.

Mwanzoni mwa mwaka huu msanii huyo wa miondoko ya R&B alikabiliwa na mashtaka 10 ya unyanyasaji wa kingono. Alikana kuhusuka na vitendo hivyo na akaachiwa huru kwa dhamana.

Ikiwa atakutwa na hatia kwa mashtaka ya awali, yaliyohusisha wanaodaiwa kuwa waathirika wa vitendo hivyo, wakiwemo wasichana wadogo watatu,atakabiliwa na kifungo cha miaka mitatu mpaka saba gerezani.

Wakili wa R.Kelly Steve Greenberg amesema mashtaka ya sasa si kwamba ni kesi mpya.

”Ameshtakiwa kwenye kesi ambayo bado ipo, ikihusisha watu walewale wanaodaiwa kuwa waathirika na muda uleule (miaka 10 iliyopita) hakijabadilika kitu”, aliandika kwenye ukurasa wa Twitter.

”Mashtaka ni yale yale ni kwamba tu yametolewa kwa nyakati tofauti, wadai ni walewale, muda ni ule ule, ushahidi ni uleule.Tunatarajia matokeo yaleyale.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu