Gwiji wa muziki wa miondoko ya RnB R.Kelly huwenda akahukumiwa kifungo cha miaka 195 Jela kwa makosa 13 ya kesi za kingono zinazomkabili.
Gwiji huyo alipandishwa kizimbani siku ya Jana Agosti 4, 2019 katika Mahakama ya Brooklyn ili aweze kufanya utetezi wa kesi hizo zinazomkabili zikiwemo kunyanyasa, kuzalilisha, na kushambulia kingono Wanawake pamoja na kurekodi watoto wadogo kanda za ngono.
Baada ya kupandishwa kizimbani siku ya Jana mahakama iliahirisha kesi hiyo na waendesha mashtaka wa kesi hiyo wamesema, Gwiji huyo atarudishwa tena Mahakamani September 14, kama akikutwa na hatia atapata adhabu ya kifungo cha miaka 195 jela.
R.Kelly amenyimwa dhamana na amerudishwa mahabusu huku Wanasheria wake wakisema mteja wao amenyimwa haki ya msingi ya kupatiwa dhamana.