Rafa Benitez akataa kurithi mikoba Goodison Park.

In Kimataifa, Michezo

Rafa Benitez amekataa ofa ya kujiunga na klabu ya Everton, ambayo inatajwa kuwa mbioni kumtimua kazi meneja wao wa sasa Ronald Koeman, kufuatia matokeo mabaya yanayoendelea kuwaandama.

Benitez alikua wa kwanza kwenye orodha ya mameneja wanaopigiwa chepuo kuchukua nafasi ya ukuu wa benchi la ufundi huko Goodison Park, kutokana na kuwa na uzoefu wa kutosha katika ligi ya England.

Benitez mwenye umri wa miaka 57 ametangaza msimamo huo, kwa kuamini bado ana nafasi ya kuendelea kudhihirisha ubora wake akiwa na kikosi cha Newcastle Utd, ambacho alikirejesha ligi kuu msimu uliopita kikitokea ligi daraja la kwanza.

Benitez anaendelea kukumbuka ka kazi nzuri aliyoifanya akiwa na liverpool mwaka 2005, na kufikia mafanikio ya kutwaa ubingwa wa barani Ulaya kwa kuifunga AC Milan.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu