Raia wa Venezuela wamepiga kura yenye utata ya kulichagua bunge maalum.

In Kimataifa

Raia wa Venezuela wamepiga kura yenye utata ya kulichagua bunge maalum litakalo ibadilisha katiba ya nchi hiyo. Hata hivyo uchaguzi huo kwa kiwango kikubwa ulisusiwa na wananchi na uligubikwa na ghasia zilizosababisha mauaji.

Kwa mujibu wa habari watu wasiopungua tisa waliuwawa katika mji mkuu wa Caracas na sehemu nyingine za nchi hiyo. Rais Nicolas Maduro amesema uchaguzi huo una lengo la kuutatua mgogoro wa kiuchumi na kisiasa nchini Venezuela lakini wapinzani wa serikali wanasema kura hiyo itaua demokrasia katika taifa hilo la Kusini mwa Amerika.

Marekani, Colombia, Panama,Peru na mashirika kadhaa ya kimataifa yamesema hayatotambua matokeo ya kura hiyo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu