Leo January 8 kutoka Ikulu jijini Dar Es Salaam Rais Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya mawaziri, lengo likiwa ni kutaka kuleta maendeleo kwa uharaka na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Akizungumza mbele ya wanahabari Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema kuwa, Rais Magufuli amemteua Mh Dotto kuwa waziri kamili wa madini na kumuhamisha Mh Angela Kairuki kwenda ofisi ya waziri mkuu na kushika kitengo cha uwekezaji, lakini pia Balozi Kijazi amesema Rais Magufuli amefungua ubalozi nchini Cuba.