Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Thobias Mwesiga ambaye aliteuliwa mapema hapo jana, kufuatia utenguzi huo Rais Samia amemrejesha Dkt.James Mataragio kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo.
Hapo awali Dkt. Mataragio ndiye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TPDC kabla ya uteuzi wa Mwesiga kutangazwa jana Jumapili Aprili 4, 2021.