Kufuatia janga la kuungua moto soko kuu la Kariakoo wafanyabishara waliokuwa wakifanya biashara katika soko kuu la Kariakoo kuhamia katika masoko mengine kama Kisutu,Machinga Complex na mengine na jana ulimskia Mkuu wa Mkoa wa DSM baada ya kutembelea soko hilo na kusema wafanyabiashara waliokuwa Kariakoo kutolipa ushuru kwa miezi miwili na hicho ndicho kifuta machozi kwao.
Sasa leo Rais Samia Suluhu Hassan ametoa milioni 100 soko la machinga Complex kwa ajili kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya biashara zao katika sehemu nzuri wakiwemo na wale waliotoka Kariakoo.