Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la watu wa
Ethiopia Sahle Work Zewde,amewasili nchini Tanzania tayari
kufanya ziara ya kikazi ya siku moja wilayani Chato.
Rais Work Wezde amepokelewa katika uwanja wa ndege wa
Geita Chato saa nne asubuhi na mwenyeji wake Rais Dkt John
Baada ya mapokezi hayo waliambatana hadi Ikulu ndogo ya
Chato kwa mazungumzo ya faragha na kisha kuendelea na ratiba
nyingine zilizokuwa zimepangwa.
Mtaa wa mastory kwa uzuri tumeinasa sauti ya Rais Magufuli
akizungumza mara baada ya kumpokea mgeni wake na kueleza
mahusiano ya Tanzania na Ethiopia kuwa ni mazuri.
Kwa upande mwingine rais Magufuli amesema kuwa Tanzania
inawafungwa 1,789 kutoka Ethiopia ambao wanaoingia Nchini
kinyume na sheri, hivyo amemezungumza na rais mwenzie ili
kuwaruhusu warudi kwao, na kwa kuzingatia undugu wetu an
Ethiopia wataruhusiwa bila masharti hata waliofungwa leo.