Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameonya mahakama nchini humo akiitaka kutousaidia upinzani na kuhujumu uchaguzi unaokuja.

In Kimataifa

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameonya mahakama nchini humo akiitaka kutousaidia upinzani na kuhujumu uchaguzi unaokuja.

Uchaguzi wa urais utafanyika mwezi ujao ambapo uhuru Kenyatta anataka kuchaguliwa tena.

Siku ya Ijumaa, kufuatia kesi iliyowasilishwa mahakamani na upinzani, mahakama kuu iliamrisha tume ya uchaguzi isichapishe makaratasi ya kupigia kura.

Bwana Kenyatta alisisitiza kuwa uchaguzi huo utafanyika jinsi ulivyopangwa,.

Amesema kuwa mahakama hauwezi kudai kuwa huru na kutumia uhuru huo kuingilia idara zingine za serikali.

Muungano wa upinzani wa Nasa ulidai kuwa rais alikuwa na uhusiano na kampuni ya Dubai la Al Ghurair ambayo ilishinda zabuni ya dola milioni 24 kuchapisha makatasi hayo.

Hata hivyo Jaji mkuu wa Kenya David Maraga, ametoa onyo kwa Rais Uhuru Kenyatta kutohujumu imani ya umma juu ya mfumo wa kisheria.

Nayo tume ya Uchaguzi nchini Kenya IEBC leo inatarajiwa kukutana na wagombea wote wanane wa kiti cha uraisi akiwemo Rais Uhuru Kenyata.

Mawakili wa Tume hiyo pia watafika mbele ya mahakama ya rufaa kupata ufafanuzi zaidi juu ya uamuzi huo

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu