Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin

In Kimataifa

Rais wa Marekani Donald Trump alikuwa na mkutano wa pili na Rais wa Urusi Vladimir Putin wakati wa mkutano wa kilele wa viongozi wa kundi la G20 uliofanyika Ujerumani mwezi huu, ambao awali haukuwekwa wazi.

Viongozi hao wawili walikutana rasmi kwa mara ya kwanza kwa mazungumzo ya masaa mawili Julai 7 mbele ya vyombo vya habari vya dunia.

Baadaye Trump alisema Putin alikanusha madai kwamba Urusi iliingilia kati uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 2016.

Katika mazungumzo yao ya pili ambayo hayakuwekwa wazi awali, Trump na Putin walizungumza kwa zaidi ya saa moja nzima wakiwa pamoja na mkalimani wa Putin.

Mbali na kuwepo kwa wasiwasi kwamba Urusi ilihusika katika kumuweka madarakani Trump, Ian Bremmer, Rais wa Kundi la kimataifa la ushauri wa kisiasa, Eurasia, ameliambia gazeti la Marekani la The Hill kwamba Trump kushiriki mazungumzo hayo bila ya kuwepo mkalimani wake ni kukiuka itifaki ya usalama wa kitaifa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu