Rais wa Sudan avunja serikali yake.

In Kimataifa

Rais wa Sudan Omar la Bashir jana amevunja Baraza lake la Mawaziri na kumchagua Waziri mkuu mpya ikiwa ni hatua ya kukabiliana na mzozo wa kiuchumi uliokumba nchi yake katika miezi ya hivi karibuni.

Amemteua Motazz Moussa kuwa Waziri mkuuu mpya wa nchi hiyo, ambaye anashika nafasi ya Bakri Hassan Saleh aliyechaguliwa kuongoza nafasi hiyo mwaka 2017.

Kabla ya kuteuliwa katika nafasi yake hiyo, Motazz Moussa alikuwa ni Waziri anayeshughulikia masuala ya umeme na umwagiliaji.

Uamuzi huo umekuja mara tu baada ya Rais Omar al Bashir kuitisha kikao cha dharura cha maafisa wa chama tawala katika makaazi yake katika kipindi ambacho wasiwasi wa hali ya kuuchumi imekuwa ikiongezeka kutokana na kupanda bei za vitu na vingine kutopatikana.

Hakuna nafasi nyingine za mawaziri zilizotangazwa , lakini idadi ya mawaziri katika serikali mpya itapungua mpaka 21 kutoka 31, hatua ambayo inalenga kupunguza matumizi.

Awali Naibu Mwenyekiti wa chama tawala nchini humo cha National Congress Faisal Hassan amewaambia waandishi wa habari kwamba Mawaziri wa Mambo ya Nje, ulinzi na masuala ya Rais watabaki katika nafasi zao, litakapoundwa baraza jipya la mawaziri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu