Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

In Kimataifa

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema nchi yake haitarudi nyuma katika vita dhidi ya magaidi na wapiganaji wengine wa kijihadi nchini Mali na katika eneo la Sahel.

Macron ametoa kauli hii nchini Mali baada ya kuwatembelea wanajeshi wa Ufaransa katika kambi yao ya Gao Kaskazini mwa nchi hiyo.

Akiwa na rais wa nchi hiyo Ibrahim Boubacar Keita, Macron ameongeza kuwa Ujerumani pia itaendelea na nchi yake kuhakikisha kuwa magaidi hao wanashindwa.

Aidha, amesema kuwa ushirikiano wa Ufaransa na Ujerumani ni muhimu sana barani Ulaya katika maswala ya usalama lakini pia kulisaidia bara la Afrika.

Ufaransa imewatuma wanajeshi wake 1,600 Kaskazini mwa Mali kupambana na magaidi Kaskazini mwa nchi hiyo.

Hii imekuwa ni ziara ya kwanza ya rais huyu mpya barani Afrika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu