Rais wa Uturuki ndiye aliyekuwa mpambe katika harusi ya Mesut Ozil

In Kimataifa

Rais Recep Tayyip Erdogan alimsaidia mchezaji wa Arsenal Mesut Ozil kufunga ndoa na mpenziwe mjini Instabul Uturuki

Ozil, ambaye chimbuko lake ni Uturuki, ali zuahisia kali alipopiga picha na rais wa Uturuki Erdogan kabla ya kombe la dunia mwaka uliopita.

Baadaye alistaafu katika soka ya kimataifa , akidai ubaguzi wa rangi na kutoheshimiwa baada ya picha hizo kusambaa nchini Ujerumani.

Kiungo huyo wa Arsenal alimuoa mpenzi wake malkia wa urembo wa Uturuki Amine Gulse , katika hoteli moja ya kifahari karibu na kingo za mto Bosphorus.

Wanandoa hao walianza kuchumbiana 2017 na kutangaza kilichokuwa kikiendelea kati yao mwezi Juni 2018.

Ozil alitangaza mwezi Machi mwaka huu kwamba alimuomba rais Erdogan kuwa mshenga wake swala ambalo lilizua hisia kali nchini Ujerumani.

Helge Braun, waziri wa Chansela wa Ujerumani Angela Merkel aliambia gazeti la Bild kwamba ilikuwa uchungu sana kumuona Ozil akimchagua kiongozi kama huyo baada ya shutuma alizopata na rais huyo wa Uturuki mwaka uliopita.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu