Rais Recep Tayyip Erdogan alimsaidia mchezaji wa Arsenal Mesut Ozil kufunga ndoa na mpenziwe mjini Instabul Uturuki
Ozil, ambaye chimbuko lake ni Uturuki, ali zuahisia kali alipopiga picha na rais wa Uturuki Erdogan kabla ya kombe la dunia mwaka uliopita.
Baadaye alistaafu katika soka ya kimataifa , akidai ubaguzi wa rangi na kutoheshimiwa baada ya picha hizo kusambaa nchini Ujerumani.
Kiungo huyo wa Arsenal alimuoa mpenzi wake malkia wa urembo wa Uturuki Amine Gulse , katika hoteli moja ya kifahari karibu na kingo za mto Bosphorus.
Wanandoa hao walianza kuchumbiana 2017 na kutangaza kilichokuwa kikiendelea kati yao mwezi Juni 2018.
Ozil alitangaza mwezi Machi mwaka huu kwamba alimuomba rais Erdogan kuwa mshenga wake swala ambalo lilizua hisia kali nchini Ujerumani.
Helge Braun, waziri wa Chansela wa Ujerumani Angela Merkel aliambia gazeti la Bild kwamba ilikuwa uchungu sana kumuona Ozil akimchagua kiongozi kama huyo baada ya shutuma alizopata na rais huyo wa Uturuki mwaka uliopita.