Riek Machar atoa wito wa kuanza upya mazungumzo ya amani nje ya taifa linalokumbwa na vita la Sudan Kusini.

In Kimataifa
Kiongozi wa upinzani aliyeko uhamishoni Riek Machar ametoa wito wa kuanza upya mazungumzo ya amani nje ya taifa linalokumbwa na vita la Sudan Kusini.
Machar ametoa taarifa hiyo hapo jana kupitia mpatanishi wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa, ambapo pia alikataa kukemea machafuko yanayoendelea nchini humo au kutangaza usitishwaji wa mapigano kutoka upande wake.
Hii imetokea wakati Marekani ikiwaonya viongozi nchini Sudan Kusini kuwa wako katika hatari ya kupoteza msaada wa Marekani kama watakataa kushiriki katika mazungumzo ya amani na kuheshimu muda uliowekwa wa kusitishwa mapigano.
 Maelfu ya watu wameuawa na zaidi ya milioni 3.5 wamekimbia makazi yao baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu aliyekuwa naibu wake Machar kwa kupanga njama ya mapinduzi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu