Zaidi ya shilingi milioni tisini 90 zimetolewa na shirika lisilo la kiserikali nchini Marekani SEE WAY kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 6 na ukarabati wa matundu 16 ya vyoo katika shule ya msingi Embasenyi iliyopo Wilaya ya Arumeru Mashariki Mkoani Arusha.
Akizungumza na vyombo vya habari mapema leo Diwani wa kata hiyo mh. Gadiel Mwanda amesema ujenzi huo ulianza mwaka 2018 ambapo lengo lilikuwa ni kuondoa changamoto ya wanafunzi wengi kwenye darasa moja ikiwa ni pamoja na umbali mrefu kwa wanafunzi hao
Amewataka Wazazi na walezi wa kata ya Embasenyi kushirikiana na Walimu ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza watoto wao kusoma kwa bidiii ili waweze kufikia malengo yao ya badae.
Hata hivyo amesema kuwa miradi mbalimbali itaendelea kuimarishwa ndani ya kata hiyo lengo likiwa ni kuleta maendeleo kwa wananchi na kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana.