Serena Williams agaragazwa na dada yake michuano ya Indian Well.

In Kimataifa, Michezo

Mchezaji tennis raia wa Marekani mwanadada, Venus Williams amefanikiwa kumfunga mdogo wake, Serena Williams hatua ya raundi ya tatu ya michuano ya   Indian Wells na kuwa mwisho wa safari yake toka kurejea baada ya uzazi.

Mchezaji huyo aliyewahi kuwa namba moja katika viwango vya ubora duniani amepoteza mchezo huo kwa jumla ya seti 6-3 6-4.

Baada ya matokeo hayo, Serena Williams ambaye kwa mara ya mwisho amefungwa na dada yake, Venus mwaka 2017 katika michuano ya wazi ya Australia amesema kuwa bado safari yake ndefu na kamwe si yarahisi.

Baada ya ushindi huo Venus anafanikiwa kusonga mbele hadi raundi ya 16 ambapo atakabiliana na  Anastasija Sevastova ambaye amemfunga, Julia Goerges kwa seti  6-3 6-3.

Serena amerejea katika mchezo huo baada ya kutoka katika uzazi wa mwanawe, Alexis Olympia tarehe 1 ya mwezi Septemba mwaka 2017 wakati alipo mfunga, Venus kwa seti 6-4 6-4.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu