Serikali kuanza kuwatambua wazalishaji wadogo wa umeme.

In Kitaifa

Serikali imesema itaanza kuwatambua wazalishaji wadogo wa umeme na kuwasimamia, hata kama wanazalisha umeme kwa kiasi kidogo .

Hayo yamesemwa  jijini Dodma Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ,wakati wa kikao baina yake na watumishi wa Tanesco na wa mradi wa umeme vijijini REA.

Dkt.Kalemani amesema kuwa ni wajibu wa Tanesco na REA kuwatambua wazalishaji wadogo wa umeme,  ifike mahali ufanyike utafiti unaoweza kusaidia kuongeza umeme, na wale  wenye  leseni za EWURA.

Aidha amesema kuwa watendaji hao wameitwa ili kutafakari walichokifanya 2018/2019, na kujipanga upya kutekeleza majukumu yao katika mwaka wa fedha unaoanza julai ili kuhakikisha huduma  zinakuwa imara muda wote.

Aidha amewataka kusimamia suala la kupeleka umeme kwenye taasisi kama vyuo, shule, makanisa, hospitali na taasisi nyingine ,zikaweze kusaidia jamii ya maeneo husika.

Waziri Kalemani ametaja baadhi ya  ajenda moja wapo Iliyojadiliwa katika kikao hicho, ni  utekelezaji wa kupeleka umeme vijijini  kwa nchi nzima.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu