Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) itajenga kiwanda cha viatu kinachomilikiwa na vikosi vya SMZ na mwaka wa fedha 2017-2018 imetenga zaidi ya sh bilioni 1.3.

In Kitaifa

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) itajenga kiwanda cha viatu kinachomilikiwa na vikosi vya SMZ na mwaka wa fedha 2017-2018 imetenga zaidi ya sh bilioni 1.3.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara maalumu ya vikosi vya SMZ, Haji Omar Kheir amesema maandalizi ya kukiwezesha kiwanda cha kutengeneza viatu na vifaa vya wapiganaji ikiwemo sare yamekamilika.

Amesema maandalizi hayo yamekamilika baada ya Baraza la Mapinduzi kuridhia mpango huo ulioifanya Wizara ya Fedha na Mipango kutenga fedha za ujenzi huo.

Aidha amesema uamuzi wa kujengwa kwa kiwanda hicho unatokana na ushauri wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein kwa vikosi vya ulinzi kuwa na vifaa vya kisasa.

Amesema kamati ya matayarisho ya ujenzi wa kiwanda imefanya ziara katika nchi mbalimbali kujifunza uendeshaji wa kiwanda.

Amevitaja vikosi vitakavyofaidika na ujenzi wa kiwanda hicho kuwa ni Valantia, Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU), Kikosi cha Kupambana na Magendo (KMKM), Chuo cha Mafunzo na Idara ya Zimamoto.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu